Saturday, November 30, 2013

MAHAFALI YA 15 YA CHUO CHA MTAKATIFU AUGUSTINO (MWANZA) HII NI TASWIRA KATIKA PICHA

Katika mahafali hayo jumla ya wahitimu 3091 wamehitimu katika vitivo mbali mbali , huku wengi zaidi ya 800 wakishindwa kuhitimu kutokana na sababau mbali mbali zikiwemo kushindwa kufisha alama stahiki za ufaulu katika mihula yao mbali mbali.
Shughuli hiyo ilianza kwa ibaada ya misa takatifu, ambapo wahitimu na wanajumuiya wengine walihudhuira misa hiyo ambayo iliongozwa na Baba Askofu Niwemugizi wa jimbo la Lulenge Bukoba.
Aliyetunuku vyeti stashahada , shada na shahada za uzamili alikuwa ni makamu wa rais wa baraza la maaskofu katoliki (TEC) Askofu Niwemugizi wa jimbo katoliki la Bukoba. Wageni wengine mahususi walikuwa ni pamoja na jaji mkuu mstaafu jaji Agustino Ramadhani, na majaji wengine wa kanda ya mwanza, viongozi wa serikali.
Yafuatayo ni baadhi ya matukio katika picha..


Picha ya kwanza na ya pili katika misa takatifu. Picha ya tatu ni Jaji Agustino  Ramadhani akishiriki katika Misa hiyo
Hitimisho la misa takatifu. Picha ya chini ni brass band ikiongozi wahitimu na wahadhri pamoja na jukwaa kuu kuingia uwanjani katika mahafali



Ndugu zangu katika taaluma wakijitahidi kuweka mambo sawa

President wa wanafunzi Bwana Dova akitoa neno kidogo

Maaskofu Niwemugizi (Kulia) na Askofu Ndimbo wakiendelea kutafakari na kufuatilia mambo katika mahafali hiyo

Makam mkuu wa chuo SAUT Dkt Pius Mgeni akitoa neno katika kusanyiko hilo


Kijana wangu kutoka radio SAUT FM Martini Nyoni ... akinukuu machache wakati alipoongoza matangazo ya moja kwa moja 


Hoyce Temu katika mahojiano na radio SAUT FM mapema leo




Mhariri mkuu wa kwa Neema Fm, ya Mwanza Bwa Jeston Kihwelo akiwa na wake wa ubani mara baada ya kuhitimu shahada ya mawasiliano ya umma

2 comments:

Unknown said...

Kazi nzuri

Elia said...

Karbu sana kaka Dova