Saturday, December 15, 2012

SERIKALI: HATUKO TAYARI KUONA DAWA FEKI ZINAZAGAA

Story ya Idrisa Bandali, Mtwara

Serikali imesema haiko tayari kuona dawa feki na bandia zikiendelea kusambazwa na kuathiri maisha ya wananchi watumiaji wab dawa hizo.
Kauli hiyo imetolewa hii leo na katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw Rashid Pagisa alipokuwa anafungua semina ya siku moja ya waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Lindi na mtwara iliyofanyika katika ukumbi wa bandari na kuandaliwa na Mamlaka ya chakula na dawa Nchini TFDA
Bw Pangisa amesema kuwa kuendelea kufumbia macho wasambazaji wa dawa hizo feki (duni) ni kuhatarisha maisha ya wananchi walio wengi
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu TFDA Nchini Bw Hiiti Sillo amewataka waandshi wa habari kutumia taaluma zao kuwaelimisha wananchi juu ya matumizi ya dawa bora na zenye viwango.

No comments: