Thursday, November 8, 2012

SUGU KUINGILIA VURUGU ZA MAFUTA MBEYA


Story ya www.dankaijage.blogspot.com
MBUNGE wa mbeya Mjini Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Sugu amesema kuwa kwa sasa nguvu zake za kutuliza vurugu za watu wanaotaka kuteka magari ya mafuta jijini hapo.
Mbilinyi amesema kuwa kutokana na tatizo la mafuta nchini wakazi wa jiji la Mbeya kwa sasa wameanza fujo za kutaka kuteka magari ya kusafirisha mafuta kwenda nchi za jirani.
Kwa mujibu wa Mbilinyi alisema kuwa hali hiyo inatokana na msimamo wa serikali kudai kuwa hakuna tatizo la mafuta nchini wakati katika jiji la Mbeya tatizo hilo ni kubwa na kupelekea nauli ya daladala kupanda ktoka shilingi 500 hadi kufikia shilingi 1500.
“Mimi kama mbunge jiji Mbeya ambaye nimekuwa nikijitahidi sana kutuliza ghasia za wananchi wangu pindi inapotokea machafuko kwa hili sasa nimeshindwa” alisema Sugu.

Mbali na hilo alisema hali hiyo inasababishwa na serikali kutokuwa na uwazi katika masuala mazima ya kutoa taarifa za ukweli kwa wananchi na pale inapotokea matatizo kama hayo.
Hivi karibuni ulitokea sokomoko kubwa ambalo lilipelekea kuzuka kizaa zaa bungeni.
Kutokana na kizaa zaa hicho cha mafuta kilipelekea, WAZIRI kivuli wa Nishati na Madini, John Mnyika , kuibana serikali akitaka itoe kauli kuhusu uhaba wa nishati ya mafuta uliyoikumba nchi, baada ya kushindwa kufanya hivyo licha ya kuwa iliahidi.
Pia ilipelekea hoja hiyo ilitikisa bunge  baada ya Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Kangi Lugola, alipoibua hoja ya kutaka Bunge lisitishe shughuli zake na badala yake wabunge wajadili tatizo hilo.
Pamoja na hoja hiyo ya Lugola na Maelezo mazuri ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene kwamba tatizo hilo limekwisha,  Spika wa Bunge, Anne Makinda alimuagiza Waziri wa Nishati na Madini kulitolea tamko rasmi suala hilo jana.
Hata hivyo katika hali ya kushangaza, serikali ilishindwa kutoa tamko huku Waziri wa Nishati na Madini pamoja na Naibu wake wote wakiwa hawapo Bungeni.
Kutokana na kushindwa huko kwa serikali, hali hiyo ilimlazimu Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo kuomba muongozo  akitumia Kanuni ya Bunge ya 68 (7)  kuhoji  kwa nini serikali imeshindwa kuliweka suala hilo kwenye ratiba ili Mawaziri watoe tamko kuhusu tatizo la mafuta.
Pamoja na hilo, Mnyika alimshutumu Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Simbachawene kwa kulieleza Bunge uongo kwamba tatizo la mafuta limekwisha wakati bado lipo.
“Napigiwa simu na watu wananiambia kwamba tatizo la mafuta bado lipo, Waziri alieleza uongo kwamba tatizo la mafuta hakuna naomba serikali ieleze kuhusu hilo” alisema Mnyika.
Mbali na hilo Mnyika pia aliwashangaa Waziri wa Nishati na Madini, Sospeter Muhongo kutofautiana kauli na Naibu wake, Simbachawene  kuhusu kumalizika kwa tatizo hilo huku mwingine akisema bado.
Baada ya kauli hiyo ya Mnyika, ilimlazimu Spika Makinda kumpa nafasi Waziri Mkuu alitolee ufafanuzi kutokana na kutokuwepo kwa  Waziri wa Nishati na Madini wala Naibu wake.
Kuhusu hilo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliahidi serikali kutoa tamko kabla ya shughuli za Bunge hili hazijakwisha.
Pamoja na hilo Pinda pia alikiri Waziri wa Nishati na Madini pamoja na Waziri wake kutoa kauli za kutofautiana  huku akilihakikishia Bunge kuwa serikali itatoa kauli yake.
Hata hivyo Pinda alisema kuwa tatizo la mafuta mikoani lisigeweza kumalizika kwa siku moja au mbili kwa sababu matanki yakijazwa na yakianza kupelekwa huchukua muda kidogo.
Ijumaa iliyopita wakati Mbunge Lugola akitoa hoja yake ya kutaka Bunge lijadili tatizo la mafuta alisema hali ya upatikanaji wa mafuta jijini Dar es Salaam na baadhi ya mikoa imekuwa mbaya, kiasi cha kuwafanya watu kupata nishati hiyo kwa vibaba.
Lugola alisema ana wasiwasi na  tatizo linachochewa na hujuma inayofanywa na baadhi ya wafanyabiashara wa mafuta ambao wanataka kukwamisha mpango wa Serikali wa kuagiza mafuta kwa pamoja (Bulk Procurement).
                               
“Hujuma zinafanyika kuonyesha mfumo wa ununuzi wa namna hii si mzuri ili Serikali irudi  kwenye mfumo wa zamani wa kuagiza  mafuta ya reja reja ili wao wafaidike zaidi.

“Ninaomba Bunge lako tukufu liahirishe shughuli zake ili tuweze kujadili jambo hili na ninaomba wabunge wote waniunge mkono”.
Hoja hiyo ilipoungwa mkono, Spika wa Bunge, Anne Makinda alimtaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kutoa kauli ya Serikali juu ya tatizo hilo.
Hata hivyo kauli ya Serikali ilitolewa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene ambaye alisema tatizo hilo limekwishashughulikiwa.
Wakati akitoa kauli hiyo jana, Profesa Muhongo hakuwapo bungeni kwa maelezo kuwa yupo Dar es Salaam akijadiliana na wadau wa mafuta katika kutatua tatizo hilo.
Akielezea chanzo cha tatizo hilo, Simbachawene alisema ni uzembe uliofanywa na baadhi ya watendaji katika Idara, Mamlaka na Taasisi za Serikali zilizopewa jukumu la mafuta.
Aliwataja wanaohusika na uzembe huo ni Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mratibu wa ununuzi wa mafuta kwa jumla (PIC).
Simbachawene alisema watendaji hao waliruhusu meli zenye mzigo wa mafuta kwa ajili ya nchi jirani kutia nanga bandarini, bila kujua kiwango cha akiba ya mafuta kilichopo hapa  nchini.
“Tatizo hili tumelishughulikia tumechukua mafuta yaliyokuwa yakipelekwa nchi jirani na kuyafungulia hivi sasa Dar es salaam imekwishajaa mafuta na sasa yanatoka huko na kwenda mikoani” Alisema na Spika kumtaka atoe kauli ramsi ya serikali jana.

No comments: