Tuesday, October 2, 2012

WAZEE VUTENI SUBIRA


Story ya Ahmad Nandonde,

Wazee Mkoani Mara Wametakiwa Kuwa Na Subira Na Kuwa Na Imani Na Serikali Wakati Matatizo Yao Yikifanyiwa Kazi.

Hayo Yamesemwa Na Afisa Mtendaji Wa Serikali Za Mitaa Mkoani Mara Bw, Joseph Makinga Kwa Niaba Ya Mkuu Wa Mkoa Bw, John Tupa Katika Maadhimisho Ya Siku Ya Wazee Duniani Ambayo Kimkoa Yamefanyika Jana Wilayani Bunda Mkoani Mara.

Bw.Makinga Amesema Ni Wazi Kuwa Yapo Matatizo Mengi Yanayowakabili Wazee Ingawa Hayawezi Kufanyiwa Ufumbuzi Wa Haraka Kwani Mengine Yanatakiwa Kutungiwa Sheria,Sera Ikiwa Ni Pamoja Na Kutengewa Muda Wa Kutosha Kwaajili Ya Mapitio Ili Yafanyiwe Ufumbuzi Pale Inapobidi.

Aidha Amewataka Wakurugenzi Wa Serikali Za Mitaa Kuyafanyia Ufumbuzi Matizo Yaliyochini Ya Uwezo Wa Serikali Za Mitaa Kwani Hazihitaji Fedha Za Kigeni.

Hata Hivyo Bw.Makinga Amewataka  Wananchi Kuwa Na Tabia Ya Kujiwekea Akiba Ya Chakula Ili Kuepukana Na Kutegemea Chakula Kutoka Katika Mikoa Ya Jirani Huku Akiwataka Kujitokeza Mchakato Wa Maoni Wa Katiba Mpya Pindi Tume Inayoundwa Na Jaji Warioba Itakapofika Mkoani Hapa.

Awali Akisoma Risala Kwa Mgeni Rasmi Kwa Niaba Ya Wazee Mkoani Hapa Mwakilishi Wa Jumuiya Ya Saidia Wazee Bw.Salvus Duba Ameyataja Matizo Wanayokabiliana Nayo Kuwa Ni Madiwani Kutohudhuria Katika Vikao Vyao Kutokana Na Kutokuwa Na Posho.

Katika Maadhimisho Hayo Pia Wazee Wamepewa Vitambulisho Vya Matibabu Bila  Malipo Vilivyotolewa Na Mfuko Wa Taifa Wa Bima Ya Afya Mkoani Hapa.

Kauli Mbiu Katika Maadhimisho Hayo Ni Maisha Marefu Yanaashiria Ongezeko La Wazee Tuboreshe Huduma Zao.

No comments: