Story na Albert Laizer
Wananchi wa Nanyamba katika mkoa wa Mtwara wametakiwa
kujitokeza kwa wingi kutoa maoni yao juu ya mabadiliko ya katiba pindi muda
utakapofika wa kutoa maoni…
Hayo yamesemwa na mkurugenzi wa mji mdogo wa
Nnanyamba Ndg Alli Mpenye alipokuwa akifungua mdahalo kuhusu katiba uliofanyika
katika eneo hilo….
Mdahalo huo ulioandaliwa na asasi isiyo ya
kiserikali ya Mtwangonet ulikuwa na lengo la kuwaelimisha wananchi kuhusiana na
katiba ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania iliyopo hivi sasa….
Mwezeshaji wa mdahalo huo Ndg Markos Alban amesema zipo changamoto mbalimbali zinazohitaji kupatiwa
ufumbuzi katika katiba ijayo ikiwemo mikataba,umiliki wa taifa pamoja na
uhusiano kati ya dola na wananchi…
Mdahalo huo utaendelea tena kesho katika ukumbi wa
Pentekoste uliopo katika manispaa ya Mtwara mikindani na wananchi wameombwa
kuhudhuria...
No comments:
Post a Comment