Thursday, August 23, 2012

NALIENDELE MTWARA WAFANYA KONGAMANO KUHUSU ATHARI ZITOKANAZO NA SUMU KUVU "AFLATOXIN" ZINAZOTOKANA NA UHIFADHI DUNI WA KARANGA

Mtafiti mkuu wa mbegu za mazao ya mafuta , Dr Omary Mponda akielezea athari za uhifadhi mbaya wa Karanga naathari zitokanazo na uhifadhi huo

Dr Mponda akisikiliza swali kutoka kwa mdau wa mkutano huo.

Waandishi wa habari wakipata neno kutoka kwa mkurugenzi wa Kituo cha Naliendele  Dr Elly.

Dr Mponda na waandishi  wa habari.
STORY KIDOGO HII HAPA....
Mkutano wa kujadili jinsi ya kuzuia sumu zitokanazo na Karanga…umefanyika mtwara leo.

Wataalamu watafiti wa mazao ya mafuta, wa kituo cha utafiti wa mbegu cha Naliendele kilichopo mkoani Mtwara, pamoja na wadau wamejadili namna ya kuweza kupambana na sumu ambayo hutokana na uyoga ambao wanautaja kwa jina la “aflatoxin”.
Mkutano huo umejadili pia namna ya kuondoa ama kudhibiti sumu kuvu.  Wataalamu wanasema sumu hiyo inasababisha ugonjwa wa kansa ya ini, pamoja na mtindio wa ubongo..
Hizi ni harakati za mwanzo hapa nchini , kwa mara ya kwanza zilianzia nchini Malawi. Madhara ya sumu hizo yamepelekea vifo vilivyoripotiwa sehemu mbalimbali, ikiwemo nchini Kenya.
Wanasema gharama za kutibu ni kubwa hivyo ni vyema wananchi wakachukua tahadhari hasa kwa kukwepa kula karanga ambazo zimeathiriwa..
Karanga zilizoathiriwa na sumu hiyo ni zile zenye UKUNGU, ambao jamii kwa muda mwingi wamekuwa wakipuuzia.

No comments: