Tuesday, September 26, 2023

UFARANSA YAKUBALI YAISHE KWA NIGER

Hatimaye, baada ya wiki kadha za vuta nikuvute, Ufaransa imesalimu amri mbele ya takwa la Niger na kutangaza kwamba, balozi wa Ufaransa nchini Niger, Sylvian Itte, atarejea Paris katika saa chache zijazo. Tangazo la Ufaransa linasema pia kuwa, wanajeshi wa nchi hiyo nao wataondoka Niger ifikapo mwishoni wa mwaka huu. Sambamba na kutangazwa kwa habari hii, Baraza la Kijeshi la Niger katika taarifa yake limeeleza kuwa, kuondolewa kwa wanajeshi wa Ufaransa na balozi wa Ufaransa nchini Niger ni wakati wa kihistoria kwa nchi hiyo na kutangaza katika taarifa yake kwamba leo tunaadhimisha enzi mpya katika njia ya uhuru na mamlaka ya kujitawala Niger. CHANZO: PARSTODAY

No comments: