Sunday, April 12, 2015

AJALI AJALI AJALI... NYINGNE TENA LEO, IMEHUSISHA BASI, FUSO

Siku angalau tatu zimepita tangu kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam kusema kuwa tochi hazitakuwepo tena barabarani, na ni baada ya madereva kugoma kupinga hoja ya kutakiwa kwenda kusoma kila baada ya miaka mitatu,  ajali zinaendelea kugharimu maisha ya raia wa taifa hili,  hii ya leo moto nao umewaka baada ya magari kugongana uso kwa uso. 
NAOMBA RADHI PICHA ZINGINE ZINATISHA KIDOGO. 
Basi la Nganga linalofanya safar Iringa Kilombero limegongana uso kwa  uso na fuso. 
Magari hayo yameteketea kwa moto baada ya kugingana huko, hii imetokea maeneo ya miliman kilomita chache kutoka Ruaha mbuyun kuelekea Morogoro. 
 Watu kadhaa wamepoteza maisha akiwemo dereva wa fuso,  vifo vingine vinatajwa kusababishwa na moto. 




No comments: