Tuesday, November 12, 2013

WAHAMIAJI HARAMU SITA WAKAMATWA MUSOMA

Story yaAhmad Nandonde, MUSOMA
Idara Ya Uhamiaji Mkoani Mara Imefanikiwa Kuwakamata Wahamiaji Haramu Sita Raia Wa Ethiopia Kwa Kipindi Cha Kuanzia Nov Mosi Hadi Hivi Sasa.
Hayo Yamesemwa Leo Na Afisa Uhamiaji Mkoani Mara Bw. Ally Dadi Alipokuwa Akizungumza Na  Mwandishi Wa Habari Hizi Ofisini Kwake.
Bw. Dadi Amesema Wahamiaji Hao Walikamatwa Wakiwa Kwenye Harakati Za Kuingia Nchini Kupitia Mpaka Wa Sirari Kuelekea Bunda Na Mwanza Kwa Kutumia Usafiri Wa Piki Piki.
Katika Tukio Hilo Amebainisha  Kukamatwa  Kwa  Pikipiki Moja  Iliyokuwa Na Namba  Za Usajili  T 861ckk Mali Ya Bw. Samwel Maduhu Mkazi Wa Bunda Mkoani  Mara
Ametaja Baadhi Ya Majina Ya Wahamiaji Hao Kuwa Ni Tekla Eriwaro, Solomon Labso  Abiwate Eldoro, Dopfe Huku Dereva Wa Pikipiki Hiyo Akikimbia Kusikojulikana.
Wahamiaji Hao Haramu Wameshitakiwa Katika Mahakama Ya Wilaya Ya Musoma Na Kesi Yao Imeahirishwa Na Raia Hao Kurejeshwa  Rumande  Baada Ya Kukosa Mkali Mani .
Pia Amebainisha  Sababu Zinazowafanya Wahamiaji Haramu Kutumia Usafiri Wa Pikipiki Ni Kutokana Na  Kuimarisha Ulinzi  Katika Barabara Kuu Na Hata Katika Vizuizi. (MSIKILIZE BWANA DADI)
Hata  Hivyo  Amewataka  Watenfaji Wa Kata, Vijiji, Wilaya Na Hata Kwa Wananchi Kuwa Na Uzalendo Kwa  Kutoa Taarifa Katika  Mamlaka Husika Pale Wanapowabaini Wahamiaji Haramu Au Wageni Ambao Wanawasiwasi Nao Katika Maeneo Wanayoishi.

No comments: