Saturday, December 8, 2012

KIBAMBA AFUNGUKIA MALIMBE MWANZA , NI KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA MPYA

HIKI HAPA ALICHOKISEMA
•Ni kazi Mpya, inayohusisha mchakato na masuala mapya.
•Ni kazi ya kutafuta suluhu na muafaka wa mambo.
•Ni suala la nipate kidogo, niachie kidogo.
•Si kazi rahisi hata kidogo kwa kuwa kuna vuta nikuvute ya nani atapata nini, atapoteza nini katika Mchakato mzima !
•Kuna vuta nikuvute kati ya mamlaka yaliyo serikali kuu na yale yaliyo serikali za Mitaa.
STORY KIDOGO.... wasomi walioko vyuo vikuu ni lazima waweze kuwasaidia wananchi wanaouzunguka vyuo ili waweze kupata faida ya uwepo wao katika maeneo vyuo vilipo, na kuweza kusaidia pamoja na kuelekeza mpangilio wa madaraka na mamlaka kuanzia serikali za mitaa ili kuwa na katiba yenye manufaa kwa umma
STORY TENA....mchakato wa ukusanyaji maoni kuhusu katiba mpya Bwana Kibamba amesema kuwa mchakato huo unaendelea vizuri ,ingawa unapelekwa kwa kasi na wanasiasa kwa kuwa wanatazama uchaguzi mkuu wa 2015
Story kidogo, Jimmy Luhende, na Kibamba
 The president wa wanafunzi, MALISA G, (kushoto)anasikiliza jambo na mdau wa GIZ.
 Ndugu mgeni mualikwa akitafakari jambo ....kama kule bungeni tu...
 Kibamba na waaandishi
Washiriki wa mdahalo huo..
KIDOGO ALICHOKISEMA MALISA....kuna haja ya wasomi kuwa na hoja muafaka wanayotaka ifanyiwe kazi katika katiba mpya badala ya kila mmoja kuwa na hoja yake binafsi ambayo hata hivyo haiwezi kusaidia jamii

No comments: