Sunday, November 25, 2012

MKOA WA MARA KESHO UNAZINDUA SIKU 16 KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA


Story ya Ahmad Nandonde , MUSOMA

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Mara kamishina msaidizi mwandamizi Absalom Mwakyoma kesho anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kwa Wanawake Mkoani Mara zinazofanyika katika kijiji cha kitaswaka kata ya Bwiregi Wilayani Butiama zilizoandaliwa na asasi isiyo ya kiserikali ya ABC Foundation chini ya ufadhiri wa Shirika la WiLDAF lenye makao makuu yake Jijijini Dar es salaam.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake,Mkurugenzi wa ABC Foundation ambalo ni shirika la kutetea haki za Wanawake na Watoto Eustus Nyarugenda amesema kuwa maandalizi yote kuhusiana na uzinduzi huo ambao lengo lake ni kuzuia na kukomesha matukio ya ukatili katika jamii yanakwenda vizuri na taari Wananchi wa kata ya Bwiregi wapo tayari kwa ajili ya kushirikiana na shirika hilo katika siku hizo 16.
Amesema kuwa kutokana na kuendelea kujitokeza kwa matukio ya ukatili huku mkoa wa Mara ukiwa unashika nafasi ya kwanza katika matukio ya ukatili anaamini siku hizo 16 itakuwa ni chachu ya kutokomeza hali hiyo na kupelekea jamii kubadilika na kuaachana na matukioa yote ya ukatili hususani kwa Wanawake.
Nyarugenda amedai kuwa kesho novemba 26 ni uzinduzi wa siku ya Kimataifa ya tunaweza kampeni ya zuia ukatili dhidi ya Wanawake ambapo shughuli kama hizo zitafanyika katika maeneo mbalimbali yan Mkoa wa Mara huku kimkoa ikifanyika Wilayani Butiama katika kata ya Bwiregi.
Amesema katika siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia Mkoani Mara wamealika mashirika mbalimbali yanayojishughulisha na ukatili wa kijinsia kutoka kanda ya ziwa kutoka mikoa ya Shinyanga,Mwanza pamoja na Bukoba huku akiwaomba wadau mbalimbali wa masuala ya kupinga mambo ya ukatili watoe ushirikiano katika kukomesha masuala ya ukatili.
Kauli mbiu ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia mkoani Mara inasema Funguka,Kemea Ukatili Dhidi ya Wanawake na sote tuwajibike.

No comments: