Thursday, October 4, 2012

MARA ACHENI KUTEGEMEA HAREMBEEE - RCC


Story na Ahmad Nandonde

Halmashuri Ya Mkoa Wa Mara Imetakiwa Kuepuka Kutegemea Harambee Kutoka Mikoa Ya Mbali Kama Vile Dar Es Salaam Badala Yake Watumie Wananchi Waishio Mkoa Huo Na Wadau Mbalimbali Wa Maendeleo  Ili Kuchangia  Harambee Ya Muendelezo Wa Ujenzi Wa Hospital Ya Kwangwa Ambayo Itaitwa Mwalimu Nyerere Memorial Hospital.

Hayo Yamesemwa  Mjini Musoma Katika Kikao Cha Ushauri Cha Mkoa Rcc  Kilichofanyika Katika Ukumbi  Wa Mkoa  Huo  Ambapo Kiasi Cha Shilingi Bilioni Tano Zinahitajika Ili Kuakamilisha Ujenzi Huo Na Tayari Serikali Imetenga Shilingi Bilioni Mbili  Kwa Ajiri Ya Ujenzi Huo Hivyo Kuwepo Na Upungufu Wa Shilingi Bilioni Tatu Ambazo Ndizo Zitakazofanyiwa Harambee.
  
Ujenzi  Na Harambee Hiyo  Unatarajiwa Kuanza Rasmi  Hivi Karibuni  Na Hii Imekuja Siku Chache Baada Ya Taarifa Ya Mkakati Wa Mkoa Wa Mara Wa Kuboresha Huduma Za Afya Za Rufaa Katika Ngazi Ya Mkoa Iliyotolewa Na Mganga Mkuu Wa Mkoa, Na Kujadiliwa Na Kikao Cha Kamati Ya Ushauri Ya Mkoa Rcc Ambapo Wajumbe Mbali Mbali Walipendekeza Hoja  Zitakazo Hakikisha Kuwa Ujenzi Huo Unaanza Rasmi Ikiwa Ni Pamoja Na Ukusanyaji Wa Fedha Za Kuendeshea Hospitali.

Sanjari Na Hayo Wajumbe Pia Waliomba Kuundwa Kwa Bodi Ya Hospital Ya Mkoa Ambayo Itatoa Msaada Mkubwa Katika Kuendeleza Huduma Za Tiba,Vilevile Uchangiaji Wa Uendeshaji Wa Hospital  Ya Kwangwa Unatarajia Kufanyika Jijini Dar  Es Salaam Na Mjini Musoma ,Ambapo Mkuu Wa Mkoa  Wa Mara Mhe John Tuppa Amemtaja Mhe Rais Kuwa Mgeni Rasmi Katika Harambee Iyo.

Kadhaika Wajumbe Wameomba Tathmini Ya Fidia Kwa Watakaoathirika Na Uendelezaji Wa Hospitali Iyo Ya Kwangwa Ifanyike Na Ukamilke Mapema Na Pia Tathmini Ionyeshe Kuwa Ni Kaya Ngapi Zitalipwa Fidia Na Kiasi Gani Cha Pesa Kitakacholipwa Kwa Kila Kaya.

No comments: