Wednesday, May 16, 2012

HOTELI YASHAMBULIWA MJINI NAIROBI

Hoteli moja maarufu visiwani Mombasa imeshambuliwa kwa maguruneti na kusababisha kifo cha mtu mmoja Hoteli hiyo ,Bella Vista Restaurant,ni maarufu sana kwa watalii na wenyeji na iko kando ya barabara kuu itokayo bandari ya Mombasa.

Hoteli hiyo ipo pembeni mwa mahali hapa.
Mkuu wa kitengo cha polisi wa jinai mjini Mombasa Bwana Ambrose Munyasya aliambia BBC kuwa watu watano walijeruhiwa vibaya katika kisa hicho.

Polisi wanasema kuwa uchunguzi wao wa awali unaonyesha kuwa kulikuwa na milipuko mitatu katika klabu hicho cha Bella Vista Restaurant.

Milipuko hiyo ilisababisha uharibifu wa magari sita yaliokuwa yameegeshwa kando ya hoteli hiyo.
Mkuu huyo wa polisi alisema kufikia sasa wanahofia kuwa shambulizi hilo lilitekelezwa na magaidi.



No comments: