Friday, February 24, 2012

Huu ndio wito wa Mkutano wa Lancaster London: 'Wasomali tumieni fursa'



Viongozi wa dunia wamewataka Wasomali kutumia ‘fursa hii adhimu’ kulijenga upya taifa lao, wakati wa mkutano maalum mjini London kujadili mustakabali wa Taifa hilo lililoharibiwa na vita.

Kumaliza vitisho vya ugaidi na uharamia ni kwa maslahi ya kila mmoja, Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron alisema.

Hillary Clinton, Waziri wa Mambo ya nje wa Marekani alisema mipango ya kuchagua viongozi na kupata katiba mpya kabla ya mwezi Agosti ni ‘kunia makuu’.

Lakini Bi Clinton alisema jukumu la serikali ya mpito inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa haitaongezewa muda wake.

Somalia imekuwa katika miongo zaidi ya miwili ya vita na njaa.

Wawakilishi kutoka makundi mengi ya Wasomali walihudhuria mkutano huo lakini kundi la wapiganaji wa kiislam wa al-Shabab linalodhibiti sehemu kubwa ya kati na kusini mwa nchi halikualikwa.

Uingereza imeielezea Somalia kama ‘taifa lililoshindwa vibaya duniani’ lakini ikasema linahitaji ‘fursa nyingine.’

Bw Cameron aliwaambia viongozi waliohudhuria mkutano huo, ambao Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan, kiongozi wa Ethiopia Meles Zenawi na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon wakiwa miongoni mwa waliohudhuria, kuwa dunia italipa gharama kubwa iwapo itapuuzia hatma ya Somalia.

"Katika nchi ambayo kuna matumaini madogo, ambapo kuna ghasia vurugu na ugaidi, na uharamia unaoharibu njia muhimu za kibiashara kuwateka watalii’ alisema.

"Mawazo ya vijana yanaharibiwa na siasa kali, kuzaa ugaidi ambao unatishia sio tu Somalia lakini kwa ulimwengu mzima. Iwapo sisi wote tutakaa tu na kuangalia, tutalipa gharama kwa kuyaacha yaendelee."

Wakati wa hotuba yake, Rais waSomaliaSheikh Sharif Sheikh Ahmed alitoa wito wa kumalizika kwa marufuku ya silaha, akisema: "Tunatafuta usalama. Tunahofu na kitakachotokea."

No comments: