Thursday, August 22, 2013

MWAKYEMBE, MAGUFULI KUADHIBIWA NA KAMATI YA BUNGE

Kutoka kwenye ukuta wa fesibuku "facebook wall" ya ZITTO KABWE 

Kimsingi Serikali ilidanganya Bunge ili Bunge lipitishe bajeti ya Wizara ya Ujenzi mwaka 2011/12. Mawaziri Magufuli na aliyekuwa Naibu yake Mwakyembe na Waziri wa Nchi Lukuvi kwa nyakati tofauti walidanganya Bunge ili kupitisha jumla ya shilingi 252 bilioni. 
PAC imeamua mawaziri hawa Waende kamati ya maadili ya bunge ili kujieleza na kuadhibiwa kwa uwongo wao. 
Magufuli - 'tunaomba fedha tshs 252 bilioni kwa ajili ya KUANZA kazi za ujenzi wa barabara' - 2011
Mwakyembe - 'fedha hizi zitachangia miradi ya wafadhili' 2011
Lukuvi - 'hizi ni fedha kwa ajili ya counterpart fund' 2011
2013
CAG - 'hizi fedha za miradi hewa na kasma kivuli'.
Magufuli - ' tulilipa madeni'
Katibu Mkuu 'tulilipa madeni'
PAC ' kwanini mlidaganya Bunge'? Mliomba fedha za kuanza miradi maalumu. Hamkuomba fedha za madeni? Kwanini mliunda kasma kivuli na kuifuta baada ya pesa kulipwa?
Uamuzi
CAG akague fedha zote za kasma hii hewa na kuripoti fedha hizi zimekwenda kwa wakandarasi gani na kutoa taarifa kwenye kamati mwezi oktoba.
Mawaziri wote waliodanganya Bungeni watashtakiwa kamati ya maadili na kudanganya bunge kwa lengo la kupitisha bajeti ya tshs 252 bilioni kufadhili miradi hewa.

No comments: