Thursday, November 8, 2012

BURIANI BALINA, WENGI WAMLILIA MWANZA

NENO LA BABA ASKOFU MKUU NORBERT MTENGA ......“hawa viongozi waliolitumikia taifa na kumwaga damu zaona  jasho lao, na wamelipenda taifa la Mungu mpaka kufa, na pengine wamedharauliwa na pengine kutokueleweka kwa sababu ya kutumikia taifa lao, hawa wote sasa wafike kwa Mungu, wakutane na Julius Nyerere na Kwa pamoja walitazame Taifa letu la Tanzania, tunawazika hawa wakati taifa letu lina mazito kweli, lina mambo ya ajabu, mambo ya kutisha na mambo ya hatari… TUFANYEJE… mkono wa Bwana utuangazie….”
<<<<<<>>>>>>>
STORY KWA KIFUPI
Mwili wa aliyekuwa Askofu wa jimbo la Shinyanga, Muashamu baba Askofu Alyosius Balina, umeagwa rasmi leo jijini Mwanza katika kanisa la Epifania Bugando,Jimbo kuu katoliki la Mwanza.
Mbele ya mamia ya waamini waliohudhuria katika Misa maalumu kwa aajili ya kumuaga mtu huyu ambaye wengi wa waliosimama walimsifu kwa juhudi za utendaji wake kiimani na katika taifa kwa ujumla, mkuu wa mkoa wa Mwanza Eng. Evarist Ndikilo , amemtaja hayati Askofu Balina kama kiongozi hodari.
Askofu Balina , alikuwa maarufu kwa utetezi wake wa vikongwe ambao wamekuwa wakiuawa kwa kile kinachodhaniwa kuwa ni wachawi, juhudi katika kupambana na mauaji hayo ikiwa ni pamoja na mauaji ya walemavu wa ngozi, Askofu Balina , alianzisha kituo cha redio kiitwacho FARAJA FM kilichopo mkoani Shinyanga.
Hayati Askofu Balina , amefariki akiwa na umri wa miaka 67, alizaliwa 1945.  Mazishi yake yatafanyika siku ya jumamosi ya tarehe 10 Novemba.
RAHA YA MILELE UMPE EBWANA, NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE,... APUMZIKE KWA AMANI!!!!
 STORY NA PICHA ZAIDI ZITAKUJIA KUPITIA  
Kanisa la  Epifania Bugando, hapa ndipo Misa takatifu ilipofanyika
Watawa (Sister) hawa nao walijumuika kumuaga mjoli wao
Jeneza lenye mwili wa Hayati Muasham Baba Askofu Aloysius Balina, hapa likiwa ndani ya kanisa la Epifania Bugando,  mchana wa leo.
Huu ndio mwili wa Marehemu Askofu Aloysius Balina, ni ndani ya Jeneza
Mapadre waliohudhuria katika Misa hiyo
Muasham Baba Askofu Thadeus Rwaichi, Jimbo kuu la Mwanza , aliongoza  Misa hiyo
WENYE SUTI NYEUSI> wa kwanza kushoto ni mkurugenzi wa hospitali ya Bugando, hospitali aliyokuwa aanatibiwa Askofu Balina hadi umauti ulipomfika, ni Dr. Majinge, anaemfuatia ni mkuu wa mkoa wa Mwanza Eng. Evarist Ndikilo. Hapa ni wakati wa misa.
Eng. Evarist Ndikilo, mkuu wa mkoa wa Mwanza, akitoa salamu za rambi rambi kwa niaba ya serikali.
“hawa viongozi waliolitumikia taifa na kumwaga damu zaona  jasho lao, na wamelipenda taifa la Mungu mpaka kufa, na pengine wamedharauliwa na pengine kutokueleweka kwa sababu ya kutumikia taifa lao, hawa wote sasa wafike kwa Mungu, wakutane na Julius Nyerere na Kwa pamoja walitazame Taifa letu la Tanzania, tunawazika hawa wakati taifa letu lina mazito kweli, lina mambo ya ajabu, mambo ya kutisha na mambo ya hatari… TUFANYEJE… mkono wa Bwana utuangazie….”   HAYA NI MANENO YA ASKOFU MKUU, MWENYEKITI WA T.E.C, Muasham Baba Askofu Norbert Mtenga (Pichani)

No comments: