WAZIRI wa fedha Mustafa Mkulo mwaka jana alitaja vipaumbele 12 katika utekelezaji wa bajeti ya serikali ya mwaka 2011/2012.
Vipaumbele vya waziri Mkulo ni kilimo/mifugo/uvuvi; elimu; nishati; miundombinu; maendeleo ya viwanda; afya; maji; ardhi/nyumba/makazi; raslimali watu; sayansi/ teknolojia; huduma ya fedha na masuala mtambuka.
Suala hapa ni je.... lipi limefanikiwa kwa kiwango gani
KWA MUJIBU WA MKULO 2011/2012 SERIKALI ILIKUSUDIA HAYA:-
2.2. Serikali inataka kufanikisha nini katika mwaka 2011/2012
Kwa ujumla, Bajeti hii imelenga kuchukua hatua za kupunguza gharama za maisha kwa
wananchi na kuchochea ukuaji wa uchumi kwa kutekeleza yafuatayo:-
A. Kuongeza ubora wa huduma za Afya na Elimu nchini kupitia:
• Kudumisha faida na mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya afya na elimu
kuboresha upatikanaji wa huduma bora zinazotolewa na sekta hizi.
B. Kuboresha tija katika uzalishaji wa mazao ya Kilimo na mfumo wa Umwagiliaji
kupitia:
• Kuhamasisha uwekezaji wa sekta binafsi katika Kilimo, • Kuimarisha Utafiti na kukuza /kuendeleza uzalishaji katika kilimo na tekinolojiia za matumizi ya mashine katika kilimo, • Kuboresha miundombinu iliyopo ya hifadhi ya taifa ya chakula na kuanzisha vituo vingine katika maeneo muhimu, • Kujenga vituo muhimu vya kuhifadhia maji (yaani; mabwawa madogo, ya kati na makubwa), umwagiliaji na miundombinu ya kupitisha maji kwa ajili ya skimu 33, • Kukarabati skimu za umwagiliaji za asili zilizopo, na vyama vya msingi vya ushirika. na • Kuendeleza na kuimarisha mashirika ya Umma.
MGAWANYO
Mgawanyo wa kisekta kama asilimia ya bajeti nzima
Elimu, 16.9, Miundombinu,20.6, Afya, 8.9, Maji, 4.6, Kilimo, 6.8, Nishati &Madini, 4 na Mengineyo, 38.3
UCHAMBUZI WA ZITTO KABWE (WAZIRI KIVULI WA WIZARA HUSIKA) MWAKA HUU 2012/2013(kwenye wordpress)
Mgawanyo wa kisekta kama asilimia ya bajeti nzima
Elimu, 16.9, Miundombinu,20.6, Afya, 8.9, Maji, 4.6, Kilimo, 6.8, Nishati &Madini, 4 na Mengineyo, 38.3
UCHAMBUZI WA ZITTO KABWE (WAZIRI KIVULI WA WIZARA HUSIKA) MWAKA HUU 2012/2013(kwenye wordpress)
Serikali inapendekeza Bajeti ya TZS 15 trilioni(USD 8.75 Billion) katika mwaka 2012/13. Uchambuzi wa vitabu vya Bajeti unaonesha kwamba mafungu ya juu 5 kwenye Bajeti ni Kama ifuatavyo;
1 Huduma kwa Deni la Taifa Tshs 2.7 trilioni(USD 1.69 Billion)
2 Wizara ya Ujenzi. Tshs 1 trilioni (USD 625 Million)
3 Wizara ya Ulinzi Tshs 920 bilioni (USD 575 Million)
4 Wizara ya Elimu Tshs 721 bilioni (USD 451 Million)
5 Wizara ya Nishati na Madini Tshs 641 bilioni (USD 400 Million)
TOTAL TZS 5.982 Trilioni(USD 3.74 Billlion)
Chanzo: Vitabu vya Bajeti kwa Wabunge
KWA MUJIBU WA ZITTO KABWE2 Wizara ya Ujenzi. Tshs 1 trilioni (USD 625 Million)
3 Wizara ya Ulinzi Tshs 920 bilioni (USD 575 Million)
4 Wizara ya Elimu Tshs 721 bilioni (USD 451 Million)
5 Wizara ya Nishati na Madini Tshs 641 bilioni (USD 400 Million)
TOTAL TZS 5.982 Trilioni(USD 3.74 Billlion)
Chanzo: Vitabu vya Bajeti kwa Wabunge
Jumla ya mafungu haya ni sawa na asilimia 40% ya Bajeti. Kwa hiyo asilimia 40% ya Bajeti yote imepangwa kwa mafungu 5 tu. Fungu lenye kiwango kikubwa zaidi ya Bajeti kuliko vyote ni fungu 22 ambalo ni malipo kwa Deni la Taifa. Pia sehemu kubwa ya fedha zilizotengwa kwa Ujenzi na Nishati ni madeni kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya miaka ya nyuma.
Hii yaweza kuwa Bajeti ya kulipa madeni zaidi kuliko Bajeti ya kuchochea maendeleo. Bajeti hii pia yaweza pia kuwa ni Bajeti ya kukopa maana jumla ya TZS 5.1 trilioni(USD 3.19 Billion) zitachukuliwa kama mikopo kwa Serikali. Mikopo ya kibiashara ambayo ni mikopo ghali sana itachukuliwa kwa wingi zaidi kuliko mwaka wa fedha uliopita.
No comments:
Post a Comment