Thursday, August 9, 2012

MAZINGIRA MAZURI YAANDALIWE KWA AJILI YA UTALII


Mkutano wa pili wa shughuli za utalii wa nchi zinazoendelea umefanyika jana mjini Zanzibar, Tanzania, na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 15 zikiwemo Marekani, Uingereza, Kenya, na Korea Kusini.

Kwenye mkutano huo, waziri wa habari, utalii na utamaduni wa Zanzibar Said Ali Mbarouk amesema, ni muhimu kwa nchi zinazoendelea kuandaa mkakati wa maendeleo ya sekta ya utalii katika miaka 20 ijayo.

Amesema nchi zinazoendelea zinapaswa kuwa na mazingira mazuri, ufundi na utamaduni vitakavyowavutia watalii na kuwataka washiriki wa mkutano huo waweze kuthibitisha mwelekeo wa maendeleo endelevu katika sekta ya utalii.

Mkutano wa kimataifa wa utalii katika nchi zinazoendelea unafanyika kila baada ya miaka miwili, na unajadili matokeo ya utafiti na uzoefu kwenye shughuli za utalii, ili kutafuta njia ya kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo katika nchi zinazoendelea..

No comments: