Aliyekuwa
Balozi wa Tanzania, nchini Italia Profesa Costa Mahalu hii leo katika MAHAKAMA
ya Hakimu Mkazi Kisutu, ameshinda kesi Uhujumu Uchumi na Kuisababishia Serikali
hasara ya Euro 2 milioni, iliyokuwa ikimkabili.
Balozi
Mahalu na aliyekuwa Ofisa Utawala wa
ubalozi huo, Grace Martin walikuwa wanakabiliwa
na mashtaka sita yakiwamo ya uhujumu uchumi na kuisababishia Serikali hasara ya
Euro 2,065,827.60, katika mchakato wa ununuzi wa jengo la Ubalozi wa Tanzania
nchini Italia.
Wadadisi wa mambo hapa nchini wanasema huenda ushindi huo wa Balozi mahalu, aliyekuwa akitetewa na wakili Mabere Marando, umechangiwa na ushahidi uliomtetea kutoka kwa Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.
Wadadisi wa mambo hapa nchini wanasema huenda ushindi huo wa Balozi mahalu, aliyekuwa akitetewa na wakili Mabere Marando, umechangiwa na ushahidi uliomtetea kutoka kwa Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.
No comments:
Post a Comment