NALIENDELE
Chuo cha utafiti wa
kilimo naliendele wametoa mafunzo kwa mabwana shamba wote wa mikoa inayolima
zao la korosho ili kuboresha zao hilo. Kwa usimamizi wa Bodi ya korosho na
Mfuko wa wakfu wa pembejeo.
Akizungumza katika
semina hiyo Dr elly kafiriti, mkurugenzi wa chuo cha utafiti wa kilimo
naliendele amesema kuwa pamoja na kuwepo
na njia za kuzuia magonjwa katika zao la korosho lakini bado tatizo ni kubwa.
Amesema kuwa wakulima
wamekuwa wanapuliza dawa mara moja badala ya kupulizia mara nne (4) kwa msimu
mmoja wa zao hilo la korosho .
Kupitia mafunzo hayo
ya mabwana shamba Ndugu kafiriti amesema
kuwa wanaimani kubwa ya kuwa wakulkima watafuata utaratibu mzuri wa kupulizia
masghamba yao kutoka kwa mabwana shamba hao waliopata mafunzo hayo
Aidha amesema kuwa kwa
kuwa hakuna uwian o mzuri kati ya dawa zinazoagizwa na serikali kupitia
usimamizi wa halmashaurio husika ndio hupelekea kuwepo kwa tatizo la kupungua
kwa pembejeo hizo
Mkurugenzi anasema kuwa
kutokana na utafiti uliofanywa wamegundua changamoto mbalimbali katika
kufanikisha kuzalishwa kwa zao hilo na ameahidi kuzifanyia kazi
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
UDHIBITI
Uthibiti wa fedha za miradi kutoka serikali kuu na
zile zinazo kusanywa na halmashauri kukamilika kwa miradi husika zimesababisha
kupata hati safi kwa mwaka 2012-2013.
hayo yamebainishwa katika kikao cha baraza la
madiwani na mwenyekiti wa halmasahuri ya wilaya mtwara Ndugu Mussa Ndazigula
alipokuwa anafungua kikao hicho kilichofanyika katika ukumbbi wa ttc kawaida
mkoani hapa
Amesema kukaguliwa kwa mara kwa mara na wakaguzi wa
mahesabu kutazifanya halmashauri kuwa na
umakini katika matumizi mabaya ya fedha za miradi zinazotolewa na serikali kuu
na zile zinazo kusanywa na halma shauri husika.
Ndugu Ndazigula amewashukuru madiwani na wakuu wa
idara kwa mshikamano walionyesha hadi kufanikisha kupata hati safi mwaka huu
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
NEWALA
Mkuu wa Wilaya ya Newala,
Christopher Magala amefungua mafunzo ya mgambo katika Kata ya Mnyambe
Wilayani Newala, mkoani Mtwara hii leo.
Akihutubia wana mafunzo ya mgambo
katika Kata hiyo ya Mnyambe, Mkuu wa Wilaya hiyo amewaasa na kuwafafanulia wana
mafunzo kwamba, mafunzo hayo ya mgambo yapo kwa mujibu wa sheria namba 147 ya
mwaka 1977 na kwa mjibu wa sheria inayounda jeshi la Wananchi (JWTZ) ya mwaka
1966 na hivyo wapuuze upotoshwaji unaotolewa na baadhi ya wananchi ambao
wamekuwa wakieneza uvumi kwamba mgambo haupo kwa mujibu wa sheria.
Aidha Magala amesema kushiriki
mafunzo ya Mgambo si lazima bali ni hiari ya mtu mwenye kujitokeza na
kujiandikisha ili kuwa mkakamavu na kupata walinzi wazuri wa amani katika
jamii.
Ndugu Magala amewataka wana mafunzo
ya mgambo kuwa mstari wa mbele na kuwa mfano katika kutekeleza sheria, kanuni
na taratibu mbalimbali za nchi kwa kuwa na nidhamu kama wanajeshi wengine mara
watakapomaliza mafunzo hayo.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewaambia
faida watakazopata mara baada ya kumaliza mafunzo ya mgambo ni pamoja na
kushirikiana na jeshi la polisi kupitia mpango wa ulinzi shilikishi/Polisi
jamii katika maeneo mbalimbali mjini na vijijini, kupewa kipaumbele pale ajira
za wanajeshi zinapotolewa na kupata ajira katika makapuni ya ulinzi:
Baada ya kufungua mafunzo ya mgambo
Mkuu wa Wilaya ya Newala ametembelea shule ya Sekondari ya Mnyambe na kuikagua
na kujionea maendeleao ya shule hiyo ya mnyambe.
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>
VIONGOZI
Viongzoi wa
kata za mayanga na naumbu wametakiwa kuhakikisha kuwa wnakuwa mstari wa mbele
katika kuboresha kiparto kwa wananchi wao
Wito huo
umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Ndugu Wilmani Kapenjama Ndile alipokuwa
anazungumza na viongozi hao mapema leo
Ndugu Ndile
amesema kuwa viongozi wanapaswa kuhakikisha wanaboresha hali ya uchumi kwa
wananchi wao kwa kuhakikisha kuwa wanawatautia soko la mazao yaom
wanayoyazalisha
Amesema kuwa
kwa muda mrefu wananchi wa mtwara wamekuwa wanategemea zaidi zao la korosho
kuwakomboa kimaisha na hivyo ameshauri kulimwa zao mbadala ambalio linasoko la
uhakika ili kuondoa umaskini na utegemezi wa zao moja kwa wakulima hao
Mkuu huyo wa
wilaya yupo katika ziara ya kujitambulisha kwa wananchi na kuona maeneo ya
kufanyia kazi tangu alipoteuliwa na Rais Kikwete kuwa mkuu wa wilaya ya mtwara.
No comments:
Post a Comment